31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Lupita kung’aa ‘Star Wars’ Desemba

Lupita-Nyong-o-a-l-avant-premiere-de-12-Years-a-Slave-au-Festival-de-la-Nouvelle-Orleans-le-10-octobre-2013_portrait_w858NEW YORK, MAREKANI

MSHINDI wa tuzo ya Black Entertainment Television ‘BET’, Lupita Nyong’o, anatarajia kung’aa kwenye filamu mpya ya ‘Star War’ ambayo inatarajiwa kuachiwa Desemba 18, mwaka huu.

Staa huyo raia wa Kenya, mwaka jana alifanikiwa kuchukua tuzo ya BET nchini Marekani pamoja na tuzo ya Oscar kupitia filamu ya ‘12 years a Slave’.

Lupita amesema kwenye filamu hiyo mpya watu watapata shida kumtambua mapema, lakini watamuelewa mwishoni, hasa kutokana na mwonekano wa mavazi yake.

“Natarajia kuonekana tena Desemba hii kwenye filamu ya Star Wars ambayo ni ‘episode’ ya saba, ni filamu ya kusisimua, watu wakae tayari kuipokea kazi hiyo,” alieleza Lupita.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles