24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

LULU DIVA: SINA MPINZANI

Na ESTHER GEORGE


MSANII anayekuja kwa kasi katika muziki wa kizazi kipya, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’, amesema hana mpinzani katika kazi zake na anaamini juhudi zake zitamfikisha alipokusudia.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Lulu Diva, alisema anaamini atafika mbali kimuziki kutokana na kuwekeza akili zake katika kazi zake.

“Napenda kile ninachokifanya, naamini nitafika mbali hivyo naona sina mpinzani kwani hakuna wa kunizuia kufika nilipokusudia, namwamini Mungu na nitafika levo za kimataifa,” alisema.

Lulu Diva alisema anapambana kuhakikisha anatoa nyimbo nzuri ambazo zina ujumbe kwa jamii na matumaini yake ni kuufikisha muziki wake nje ya nchi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles