30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

‘Kwaheri watumia simu feki nchini’

James Kilaba
James Kilaba

Na Asifiwe George, Dar es Salaam

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema watu wanaotumia simu feki wajiandae kwa maumivu kwa vile wataweza kutamba nazo hadi saa 5:59 usiku wa leo.

Itakapotimia saa 6.00 kamili usiku simu hizo ambazo hazina viwango zitafungiwa na kutotumika tena, imesema TCRA.

Akizungumza na waandishi wa habari   Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,   James Kilaba, alisema hatua hiyo ya kuzimwa  simu feki itarushwa moja kwa moja  na vyombo vyote vya habari hasa runinga.

Kilaba  alitoa hahadhari kwa k wauzaji wa vifaa vya mawasiliano ya mkononi   na mafundi simu kwamba atakayebainika kubadili namba tambulishi za vifaa vya simu adhabu yake ni kifungo kisichozidi miaka 10 au faini ya Sh milioni 30 au vyote kwa pamoja.

Alisema   mfumo huo wa elektroniki ulizinduliwa  rasmi Desemba mwaka jana na unahifadhi kumbukumbu za namba tambulishi  za vifaa vinavyoibiwa, kuharibika, kupotea au ambavyo havikidhi viwango vya matumizi katika soko la mawasiliano.

Alisema uchambuzi uliofanywa Juni 14 mwaka huu, unaonyesha   mabadiliko chanya ya idadi ya namba tambulishi ambazo zilikuwa hazina viwango kupungua kutoka aslimia tatu hadi   asilimia 2.96.

“Idadi ya namba tambulishi ambazo zimenakiliwa zimekuwa zikipungua kutoka asilimia mbili hadi kufikia asilimia 0.09 hivyo kufanya idadi ya namba tambulishi za simu halisi kuongezeka kutoka asilimia 85 hadi asilimia 96.95.

“Na idadi ya  namba  tambulishi za  simu  halisi ( IMEI) zimeongezeka na kufikia asilimia  96.95 kwa mujibu wa uchambuzi  iliofanyika   Juni  14, mwaka huu.

“…namba tambulishi za vifaa vyote vya mawasiliano vya mkononi ambavyo vimeibiwa, vimeharibika, kupotea au visivyokidhi viwango katika soko la mawasiliano havitaruhusiwa kuunganishwa kwenye mitandao ya watoa huduma kuanzia (kesho)leo,” alisema Kilaba.

Alisema katika kipindi cha kutoa elimu walikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo   uaminifu mdogo kwa baadhi ya wauzaji wa simu kwa kutoa punguzo kwa wananchi   kuwashawishi kuzinunua simu bandia kwa bei nafuu.

Alieleza changamoto nyingine kuwa ni uelewa mdogo wa wananchi katika kuitikia wito wa kuhakiki simu zao katika kipindi cha mpito.

Kilaba  alieleza faida za   mfumo rajisi  wa    namba   tambulishi (IMEI) kuwa ni kupunguza wizi kwa njia  ya simu, kuhimiza utii wa sheria  na kujenga  misingi  ya matumizi  ya simu  halisi  zisizo bandia.

TCRA  imetoa mwito kwa wale wote  wanaofanya biashara ya kuingiza simu  nchini    kuhakikisha     simu wanazoleta  zinakidhi viwango na zimehakikiwa  na Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles