31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Kitengo cha Mawasiliano DAWASA ni mfano wa kuigwa -DC Gondwe

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Godwin Gondwe amekipongeza Kitengo cha Mawasiliano na Jamii cha Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kwa ufanisi na uharaka katika kufikisha taarifa kwa Wananchi.

Gondwe ametoa pongezi hizo jana baada ya utembelea mradi wa maji Rufu uliko Temeke jijini Dar es Salaam.

“DAWASA mmekuwa mstari wa mbele katika kuupasha umma habari zinazohusu Mamlaka yenu, kwnai mnatoa taarifa kwa haraka na kwa ufanisi jambo ammbalo linapaswa kuigwa na taasisi nyingine,” amesema Gondwe.

Gondwe amezitaka Taasisi nyingine za Serikali kuiga utendaji kazi na kuwajibika kutoa taarifa kwa wakati ili wananchi waweze kupata taarifa sahihi kwa wakati sahihi na kutoka sehemu sahihi ili kujenga Jamii yenye uelewa sahihi.

“Hivyo niwapongeze na niwasihi muendelee na kasi hiyo ili kuweza kufikia malengo mliyojiwekea,” amesema Gondwe.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles