23 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Kisa ‘Pay It Forward’ Obama amuita Lamar Ikulu

Kendrick LamarNEW YORK, MAREKANI

MKALI wa muziki wa hip hop nchini Marekani, Kandrick Lamar, amemkosha rais wa nchi hiyo Barack Obama kutokana na wimbo wake wa ‘Pay It Forward’.

Awali rais huyo alidai kwamba anavutiwa na msanii huyo kutokana na wimbo wake wa ‘How Much a Dollar Cost’ ambao aliuachia mwaka jana, lakini kibao hicho kipya cha ‘Pay It Forward’ kimezidi kumchanganya rais huyo na kuamua kumuita msanii huyo Ikulu.

Obama alitumia muda wake kujadili na msanii huyo juu ya kutoa elimu kwa watoto wa mitaani kama ilivyo katika wimbo huo mpya wa msanii huyo ambao unaonekana kumgusa rais.

“Nimefurahi sana kukutana na rais, kikubwa alinipa pongezi kwa kazi zangu na amedai kwa sasa ameguswa sana na wimbo wangu wa ‘Pay It Forward’ ambao unazungumzia vijana ambao wanahangaika na maisha ya mitaani,” alisema Lamar.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles