33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

KIKI ZA MASTAA ZILIZOTINGISHA

Vanessa Mdee
Vanessa Mdee

NA CHRISTOPHER MSEKENA,

KIKI siyo kitu kigeni kabisa kwa wasanii ulimwenguni. Kutafuta jambo la kushtua na kuwafanya mashabiki wamzungumzie msanii husika kwa muda mrefu zaidi akiwa na lengo la kuachia kazi yake.

Lakini kwa baadhi ya wasanii wetu hapa Bongo hujiingiza kwenye skendo wakidhani ni kiki. Kwa kawaida kiki ni nzuri ili kumsaidia msanii kujipaisha na kuchomoa kazi yake, lakini si kwa kujiharibia kwa kashfa mbaya ambazo mwisho wake kufutika inakuwa shida.

Yes! Hapa Bongo wapo mastaa wengi ambao wametingisha kwa kiki huku wengine wakijaribujaribu. Polisi wa Swaggaz anakudondoshea kiki za mastaa zilizotingisha zaidi tangu kuanza kwa mwaka huu.

RUBY, ASLAY

Kila mtu aliongea lake ilipovuma kuwa Ruby anatoka na Aslay ambaye kiumri ni mdogo kwake. Hii ilitokea Juni 13, mwaka huu mara baada ya Ruby kuanza kutupia picha za Aslay kwa fujo kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika meneno yanayoashiria kuna mahaba mazito kati yao.

Aslay yeye alimjibu Ruby kwa jumbe tamu za mahaba na kuzidi kuwachanganya mashabiki huku wengi wakitamani kuona kama penzi hilo jipya mjini litakuwa na uzito wa kuipiku kapo ya Harmonize na Wolper iliyokuwa inatamba kipindi hicho.

Wakati watu wengi wanazidi kumiminika na kuifuatilia kapo hii ndipo Yamoto Band wakaachia ngoma yao mpya inayoitwa Suu, waliyomshirikisha Ruby.

Ikasanuka kumbe ilikuwa kiki tu. Hilo lilithibitishwa hata na meneja wao Said Fella ‘Mkubwa Fella’ a.k.a Mheshimiwa Diwani.

LINEX

“Ahsante Mungu, kuna maamuzi hayahitaji matangazo, silence speaks  volumes,” aliandika Linex kwenye ukurasa wake wa Instagram mara baada ya kutupia picha akiwa kwenye mikao tofauti na mrembo aliyedai kuwa amemuoa.

Linex alizidi kupokea pongezi kutoka kwa mashabiki waliovutiwa na tukio la yeye kufunga ndoa, uamuzi ambao ni nadra mno kwa wasanii wa Bongo Fleva.

Hali ilikuwa tofauti mara baada ya kutumia picha zilezile za harusi kutengeneza kava la ngoma yake mpya iitwayo Kwa Hela, aliyoachia mwanzoni mwa mwaka huu.

Kwa tukio hilo, Linex alijikuta akipokea matusi kutoka kwa mashabiki kwa kosa la kuchezea hisia zao lakini mbali na kadhia hiyo lengo lake la kutumia Kiki lilifanikiwa, aliapoachia ngoma yake ikapenya.

RAY KIGOSI

Vincent Kigosi ‘Ray’ alifanikiwa kuwakamata mashabiki wake kwa kutengeneza kiki yenye ‘akili’ sana. Yeye aliibuka na maelezo kuwa weupe wake ni kwa sababu anatumia maji mengi na kushiriki mazoezi.

Ray alisema hayo wakati akihojiwa na kituo kimoja cha runinga jijini Dar es Saalam. Hakuna kiki inayofikia hii tangu mwaka huu umeanza. Katika mitandano ya kijamii watu mbalimbali walipiga picha wakiwa wanakunywa wakidai wanataka kuwa weupe kama Ray!

Ile kushangaashangaa, Ray akaachia Filamu ya Tajiri Mfupi ambayo ilifanya vizuri sokoni. Pamoja na kiki hiyo, Tajiri Mfupi ni kati ya sinema bora za Kibongo zilizotoka mwaka huu.

VANESSA MDEE

“Nikupe Kiki ujulikane au siyo? Kila siku twanyamaza ndiyo mtugaragaze. Mimi siyo wale uliowazoea,” aliandika Vanessa Mdee kwenye instagram akimshambulia Shilole.

Shilole hakukaa kimya naye kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika: “Veepe jipange sana, mwenzio Igunga niliaga, sijaletwa kwa kubebwa kwenye lori, nimekuja na mbio za mwenge. We si wa magorofani na kiingereza chako cha kuunga mi ndo mtoto wa mbwa, sasa ole wako tukutane utanyooka.”

Watu wakahamishia mawazo yao kwao, kutahamaki kumbe walikuwa wanaandaa shoo Club Bilicanas, Dar. Shoo ilikuwa poa kutokana na kiki hiyo.

NEDY MUSIC

Baada ya Shilole kumwagana na Nuh Mziwanda watu walikuwa wanatamani kufahamu ni nani ataziba pengo hilo. Ghafla kijana mdogo Nedy Music akaanza kuhisiwa kutoka kimapenzi na mwanadada huyo.

Sababu kubwa iliyofanya watu waanze kuhisi kuwa kuna penzi kati yao ni picha walizokuwa wanatupia kwenye Instagram zikiambatana na maneno ya mapenzi.

Hakuna aliyemjua Nedy Music kabla ya kuwa na Shilole lakini alipata umaarufu mara baada ya kiki hiyo ya kumrithi Nuh Mziwanda, hata  alipoachia ngoma yake Usiende Mbali chini ya Ommy Dimpoz kupitia lebo ya PKP alichomoka kirahisi tu.

Na hapo ndipo ikajulikana kuwa hakukuwa na mapenzi kati yao bali ilikuwa kiki ya kutafuta mashabiki kwenye muziki huu wenye ushindani. Kwa hilo alifanikiwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles