23.3 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Kesi ya kina Mbowe kuunguruma leo

Freeman Mbowe
Freeman Mbowe

NA JUDITH NYANGE, MWANZA

SHAURI la Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe kuiomba Mahakama kubatilisha amri    polisi    kuuzia mikutano ya hadhara ya vyama vya  siasa limepangwa kuanzwa kusikilizwa leo.

Tofauti na yalivyokuwa maombi yaliyowasilishwa Juni 10, mwaka huu katika shauri la  namba 79 la mwaka 2016, mbele ya  Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza  yaliyowajumuisha washtakiwa watano, shauri la sasa litajumuisha  washtakiwa   wawili ambao ni Kamanda wa Polisi Wilaya ya Geita (OCD) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Shauri la awali   namba 79 la mwaka 2016 liliwajumuisha washtakiwa watano wakiwamo Kamanda wa Polisi Wilaya ya Geita na  Kahama, Kamishina wa Operesheni  na Mafunzo wa Jeshi la Polisi   na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Juni 14, mwaka huu,    Jaji   Mohamed Gwae,  alibaini upungufu  wa  sheria katika shauri hilo  kwa kumjumuisha Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Polisi, Nsato Mssanzya ambaye kisheria anastahili kufunguliwa mashtaka masijala kuu.

Jaji Gwae aliwasahauri mawakili wa Chadema  kurekebisha hati yao.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza jana,   Mbowe  alisema shauri hilo litaanza kusikilizwa kesho (leo)  mbele ya Jaji   Gwae.

Katika shauri hilo,  Mbowe kupitia kwa Mawakili wake, Paul Kipeja na John Malya  amewasilisha maombi manne yanayohusu kutafuta haki ya kufanya mikutano na mikusanyiko ya siasa iliyozuiliwa na  polisi Juni 7, kupitia kwa Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Polisi Makao Makuu, Nsato Mssanzya.

Mbowe   ameiomba Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kutamka kuwa  amri iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Wilaya ya Geita (OCD) kuzuia mikutano ya hadhara  iliyopaswa kufanyika Katoro na mjini Geita   kuwa  si sahihi na ni kinyume cha sheria.

“Ombi jingine  tumeiomba mahakama kutengua amri ya OCD wa Geita   aliyoitoa Juni 7, 2016 kuzuia mikutano ya hadhara ya  Chadema iliyokuwa imetangazwa na kupangwa kufanyika wilayani humo kuanzia tarehe hiyo, kwa muda usiojulikana.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles