24 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Kanye West awaomba radhi Wiz Khalifa na Amber Rose

2015 MTV Video Music Awards - Fixed ShowNEW YORK, MAREKANI

MKALI wa muziki wa hip hop nchini Marekani, Kanye West, amewaomba radhi, Wiz Khalifa na mama mtoto wake, Amber Rose, baada ya kuwashambulia kwa maneno makali.

Licha ya maneno hayo kutafsiriwa kuwa makali, pia Kanye alisema kuwa Wiz Khalifa asingeweza kumpata Amber na kuzaa naye mtoto kama asingeachwa naye.

Hata hivyo, Wiz hakujibu lolote juu ya kauli hiyo, lakini Amber alijibu kwa kumtaka asimhusishe mtoto wake katika mgogoro wao binafsi.

“Najua nitakuwa nimewakosea sana Wiz Khalifa na Amber Rose, sitamzungumzia mtoto wenu tena, nawapenda wote na nawatakia heri,” Kanye aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter.

 

 

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles