Kampuni ya Sukari ya Kilombero imefanikiwa kunyakua tuzo katika kipengele cha cha Uanagenzi na Mafunzo (Apprenticeship and Internship) huku ikishika nafasi ya pili katika kipengele cha Ushirikishwaji wa Watanzania (Local Content) na kupokea cheti cha shukrani kwa kudhamini hafla hiyo wakati wa tuzo za zitolewazo na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) zilizofanyika 2022 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.