24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

JOKATE AFUNGUKA UJIO WA RAMSEY NOUAH

Na CHRISTOPHER MSEKENA

MIAKA saba baada ya kushirikishwa kwenye filamu ya The Devils Kingdom na marehemu, Steven Kanumba, staa mkongwe wa filamu kutoka Nigeria, Ramsey Nouah, ametua tena nchini kwa malengo mengine tofauti na filamu.

Akizungumza na MTANZANIA, Jokate ambaye alikuwa mwenyeji wa Ramsey nchini, alisema msanii huyo hajaja kwa ajili ya kufanya filamu bali amekuja kama mhamasishaji wa vijana kwenye kongamano lililoandaliwa na Kampuni ya Sahara Tanzania, lililofanyika jana kwenye Ukumbi wa Creative Arts PFA uliopo karibu na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

“Hili lilikuwa ni kongamano la vijana wote wa Tanzania kuwawezesha vijana kufikia ndoto zao, kwa hiyo Ramsey alikuja kama mhamasishaji kutupa maneno tuone sisi kama vijana tunajikwamua vipi katika haya maisha na kaulimbiu yetu ni ‘My future starts with me’,” alisema Jokate.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles