29.7 C
Dar es Salaam
Sunday, April 28, 2024

Contact us: [email protected]

John Nini kutua Bongo, atangaza kolabo

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka nchini Denmark, Jonathan Nininahazwe a.k.a John Nini, amesema anatarajia kutua Tanzania mwakani kwa ajili ya kuonana na mashabiki, kufurahia utamaduni na kufanya kolabo na wasanii kadhaa.

Akizungumza na Mtanzania Digital kutoka Canada, John Nini ambaye alitamba na wimbo Iza Bella, amesema huo ni ujio wake kwa kwanza Tanzania hivyo atafurahi kukutana na mashabiki pamoja na utamaduni wa Tanzania.

“Nimeshapata uhakika sasa nitakuja Tanzania Februari, 2022 kuonana na watu wangu na kufurahia utamaduni wa Kitanzania na nitafungua milango ya kolabo na wasanii wakubwa hapo Bongo.

“Kwahiyo watu wajiandae na waendelee kutembelea tovuti yangu ya www.johnnini.com kwa taarifa zaidi za ujio wangu Afrika,” amesema msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles