24.8 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Jeshi Sudan lamshikilia Waziri Mkuu

KHARTOUM, Sudan

WANAJESHI nchini Sudan leo wamewashikilia baadhi ya vigogo wa Barala za Mawaziri, akiwamo Waziri Mkuu, sambamba na viongozi wa upinzani katika kile kilichotafsiriwa kuwa ni jaribio la kuipindua Serikali,

Waziri Mkuu, Abdalla Hamdok, alikamatwa na kupelekwa kusikojulikana baada ya kukataa agizo la jeshi kumtaka aunge mkono mapinduzi, kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Habari ya Sudan.

Huku ikikumbuka kuwa jaribio la kuipindua Serikali lilifeli mwezi uliopita, hali ya usalama nchini humo imekuwa ya kutilia shaka kutokana na uadui unaotokana na kugombea madaraka kati ya jeshi la vikundi vya kiraia.

Mwaka 2019, jeshi lilimpindua Rais wa muda mrefu, Omar al-Bashir, ambaye aliishia gerezani, lakini bado kumekuwapo na sintofahamu kuelekea uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka 2023.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles