22.5 C
Dar es Salaam
Saturday, May 11, 2024

Contact us: [email protected]

‘Jalada kesi ya Masamaki liko hatua za mwisho’

b

Na Kulwa Mzee-Dar es Salaam

JALADA la kesi inayomkabili  Kamishna wa Kodi na Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Tiagi Masamaki  na wenzake, lililopelekwa kwa Manasheria Mkuu wa Serikali (AG), liko katika hatua za mwisho.

Wakili wa Serikali, Christopher Msigwa alisema hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi,   kesi hiyo ilipokuwa inatajwa.

Msigwa alisema  jalada la kesi hiyo liko kwa AG katika hatua za mwisho hivyo aliomba ahirisho fupi na mahakama ilikubali kuahirisha kesi hiyo hadi Desemba 19 mwaka huu.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni  Haroun Mpande wa kitengo cha Mawasiliano ya Kompyuta ICT TRA, Msimamizi Mkuu Kitengo cha Ushuru wa Forodha  ICD Azam, Eliachi Mrema,  Mchambuzi  Mwandamizi  wa Masuala ya Biashara  TRA,  Hamis Omary , Meneja wa Oparesheni  za Usalama na Ulinzi  ICD, Raymond Adolf Louis  na Meneja wa Azam ICD, Ashrafu Khan.

Washtakiwa wote kwa pamoja wanadaiwa kuwa kati ya Juni mosi na Novemba 17, 2015 walikula njama kwa kuidanganya Serikali.

Wanadaiwa kudanganya kuwa  makontena 329 yaliyopo katika Bandari Kavu ya Azam (AICD) yalitolewa baada ya kodi zote kufanyika wakati  si kweli.

Katika shtaka la pili,  wanadaiwa kuwa katika kipindi hicho jijini Dar es Salaam, washtakiwa hao kwa pamoja walishindwa kutimiza majukumu yao na kuisababishia Serikali hasara ya Sh bilioni 12.7.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles