24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Jaguar aiomba Serikali ipambane na dawa za kulevya

jaguarNAIROBI, Kenya

MSANII wa muziki nchini Kenya, Charles Kanyi ‘Jaguar’, ameiomba Serikali nchini humo ianzishe mashindano ya shule ili iondoe muda wa wanafunzi kutumia dawa za kulevya.

Jaguar alisema vijana wengi wanaokimbia shule wanakimbilia vijiweni kwa sababu hakuna michezo lakini kama michezo itaanzishwa katika shule itaondoa wanafunzi kukimbilia vijiweni.

“Serikali iangalie jinsi ya kuanzisha michezo shuleni ili kuwafanya vijana wajiingize kwenye michezo hiyo badala ya kurudi mitaani na kuanza kutumia dawa za kulevya,” alisema Jaguar.

Msanii huyo aliyazungumza hayo juzi katika maafali ya nane ya chuo cha Mt Kenya University, huku akiwa mwakilishi wa chama cha kupinga matumizi ya dawa za kulevya Nacada.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles