27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

JAC kupinga mauaji ya albino Arusha

DSC_5495NA MWANDISHI WETU

KUNDI la muziki wa kizazi kipya la Jicho Angavu Crew (JAC) la Arusha linatarajiwa kunogesha onyesho la kuzuia mauaji ya albino litakalofanyika Machi 12 katika ukumbi wa UAACC, Maji ya Chai, Arusha.

Katika onyesho hilo, kundi hilo linaloundwa na vijana wanne, akiwemo kiongozi wao, Chediel Greyson ‘Pyda’, Emanuel Greyson ‘Ramsee’, Oscar John ‘Okadi’ na Fyakryus Otto ‘Days’ limeandaa wimbo wa pamoja kuhusu kupinga mauaji ya albino.

“Tumejipanga kutoa hamasa kwa wanajamii kuachana na mauaji ya ndugu zetu albino kwa kuwa kila binadamu yupo kwa sababu za Mungu,’’ alisema Ramsee.

Pia kundi hilo limewataka mashabiki wao wajitokeze kwa wingi ili kupokea ujumbe na onyesho waliloandaa kwa ajili yao.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles