24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Iran ‘yawakamata’ waliohusika katika mauaji ya mwanasayansi

TEHRAN, IRAN

Baadhi ya watu waliohusiaka katika mauaji ya mwanasayansi wa ngazi ya juu wa Iran wamekamatwa , amesema mshauri wa bunge nchini humo.

Hossein Amir Abdollahian aliiambia televisheni ya Al-Alam kwamba hakuweza kushirikisha maelezo ya watu hao kwasababu za kiusalama, lakini wahusika hawatautoroka mkono wa sheria.

Amesema kuwa kuna ushahidi wa uhusika wa Israel katika mauaji hayo. israeli haijathibitisha wala kukana kuwajibika na mauaji hayo.

Mwanasayansi huyo, Mohsen Fakhrizadeh, aliuawa karibu na mji wa Tehran tarehe 27 Novemba.

Maafisa nchini Iran wametoa ushahidi unaokinzana kuhusu jinsi alivyopigwa risasi hadi kufa alipokuwa akisafiri katika msafara wa magari kupitia mji wa Absard.

Katika siku ya shambulio, wizara ya ulizi ilisema kulikuwa na mapigano baina ya walinzi wake na watu kadhaa wenye silaha . Ripoti ya Iran iliyoelezea kauli za mashahidi ilisema kuwa ” washambuliaji kati ya watatu na wanne ” waliuawa.

Lakini Jumapili , Kamanda jeshi la Iran la -senior Revolutionary Guardsalisema silaha iliyotumia setilaiti ya intelijensia bandia ndiyo iliyofyatua gari lake

Brigadia -Jenerali Ali Fadavi aliviambia vyombo vya habaro nchini humo kuwa silaha yenye ukubwa wa lori aina ya pick-up ,liliweza kuvuta picha ya ichwa cha mwanasanyansi huyo na kukilenga kwa risasi bila kumdhuru mke wake aliyekua kando yake.

Madai hayo hayta hivyo hayakuthibitishwa na duru huru na wataalamu wa silaha za kielectroniki walishuku maelezo hayo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles