24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Hospitali ya Kairuki yaboresha huduma kupunguza msongamano wa wagonjwa

k3
Muonekano wa kitengo kipya (OPD 3) katika Hospitali ya Kairuki,Mikocheni

Hospitali ya Kairuki katika kuboresha huduma zake kwa wagonjwa imeanza kutumia kitengo kipya kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa kutwa  hususani wale wanachama wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, NHIF.

Kwa mujibu wa Afisa uhusiano wa hospitali hiyo, Arafa Juba, kitengo hicho kipya (OPD 3)  kilichopo nyuma ya Jengo kuu la hospitali mkabala na kitengo cha magonjwa ya viungo (Physiotherapy Unit), kina sehemu kubwa ya mapokezi, vyumba  mbalimbali  vikiwemo  vyumba 10 vya madaktari, maabara, duka la dawa, sehemu ya sindano na kufunga vidonda, chumba cha ultrasound, mapokezi , huduma za chanjo ya watoto (RCH), chumba cha wauguzi na duka dogo la vinywaji na vitafunwa.

k1

“Kitengo hicho kipya kitaiwezesha hospitali hiyo kutoa huduma kwa haraka na ufanisi zaidi kwa wagonjwa wasiopungua 120,000 kwa mwaka hivyo kupunguza kero ya foleni na msongamano uliokuwepo siku za nyuma,” alisema Juba.

Juba aliongeza kuwa kitengo hicho (OPD3) kitazinduliwa rasmi hivi karibuni pamoja na vitengo vipya vya kusafishia figo ( Dialysis Unit) na cha huduma za dharula ( Emergency Unit).

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles