27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

GGML yaibuka muonyeshaji bora katika maonyesho ya afya na usalama mahali pa kazi 2023

Na Mwandishi Wetu, Mtanzanias Digital

KATIKA maadhimisho ya siku ya afya na usalama mahali pa kazi  yanayoratibiwa na Wakala wa afya na usalama mahali pa kazi (OSHA), Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetangazwa muonyeshaji bora (Overall best exhibitor) miongoni mwa kampuni zote zilizoshiriki maonyesho hayo mjini Morogoro

Baadhi ya wafanyakazi wa GGML, wakiwa katika picha ya pamoja kufurahia ushindi wa muonesha bora na mbunifu bora katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi yanayofanyika mkoani Morogoro.

Pia imetangazwa kuwa mbunifu bora wa maonesho hayo yaliyoanza Aprili 26 na kutarajiwa kuhitimishwa Aprili 30 mwaka huu katika viwanja vya Tumbaku mkoani humo.

Kilele cha maonesho hayo yenye kauli mbiu Mazingira Salama na Afya ni Kanuni na Haki ya Msingi Mahali pa Kazi,” kimefanyika jana mkoani humo.


Daktari wa Kituo cha Afya cha GGML kutoka Idara ya Afya, Usalama, Mazingira na Mafunzo ya GGML, Dk. Subira Joseph akitoa huduma za matibabu kwa mmoja wa wananchi waliotembelea banda la huduma za afya la kampuni hiyo kwenye maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi yanayofanyika mkoani Morogoro.
- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles