BENDI ya muziki wa dansi nchini, FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’, inatarajia kuutambulisha rasmi wimbo wao mpya wa ‘Dada Wewe’ kwenye onyesho lao maalumu litakalofanyika sikukuu ya Pasaka ukumbi wa East 24, Mikocheni Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa fedha wa bendi hiyo, Kelvin Mkinga, alisema wimbo huo ni miongoni mwa nyimbo zao mpya watakazozitambulisha siku hiyo.
“Wimbo huu ndio utakuwa zawadi kwa mashabiki wetu ingawa tutafanya onyesho la nyimbo zetu nyingi na pia tunaahidi kutoa mabadiliko makubwa katika muziki wetu ambao utatunufaisha sisi na mashabiki wetu kwa ujumla,” alisema.