NYOTA wa filamu nchini Marekani, Eddie Murphy na mke wake, Paige Butcher, wanatarajia kupata mtoto wao wa tisa ifikapo Mei mwakani.
Kwa upande wa Murphy mpaka sasa jumla ana watoto saba ambaye aliwapata nje ya mke wake wa sasa, huku mke huyo akiwa na mtoto mmoja na akitarajia kupata mtoto huyo wa pili na kuwa na familia ya watoto tisa.
Hata hivyo, kwa upande wa mrembo huyo, ‘Paige’ ameonekana kuwa na furaha kubwa ya kupata mtoto na staa huyo wa filamu.
“Ni furaha kubwa kupata mtoto na msanii ambaye ni maarufu, sasa ni muda wangu wa kuweza kuongea katika vyombo vya habari, awali nilikuwa sifanyi hivyo kwa kuogopa kutoa habari ambazo sio sahihi,” alisema mwanamitindo huyo kutoka nchini Australia.