24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

DSTV kuwapa ulaji waigizaji wa filamu Tanzania

Barbara Kambogi
Barbara Kambogi

NA KYALAA SEHEYE-DAR ES SALAAM

KING’AMUZI cha Dstv kilicho chini ya Multchoice, kinatarajia kutoa kipaumbele kwa waigizaji Watanzania kutumia chaneli yake ya ‘Maisha Magic Bongo’ kutoa elimu ya lugha ya Kiswahili Afrika.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Barbara Kambogi alisema watakuwa wakitumia kazi za waigizaji wa Tanzania kufundisha lugha hiyo.

Barbara alisema kuwa Ijumaa ijayo wanatarajia kufanya mazungumzo na waigizaji wa Tanzania, ili kuwapa utaratibu mzima wa kuwakilisha kazi zao katika kituo chao kilichopo nchini Kenya.

“Maisha Magic Bongo ni chaneli ambayo imepata umaarufu Afrika na nje ya Afrika, watu wengi wasiojua Kiswahili wamekuwa wakijifunza kupitia filamu zinazoonyeshwa,” alisema Barbara.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles