MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nassibu Abdul ‘Diamond Platnum’, amechaguliwa kuwania tuzo iitwayo African Culture Image 2016 (ACI) ambazo ni kwa ajili ya wasanii wa Afrika.
Diamond amekuwa msanii pekee kutoka Afrika Mashariki kutajwa kuwania tuzo hizo zinazotolewa na Wanaigeria na katika tuzo hizo ametajwa katika kipengele cha msanii bora wa kiume wa mwaka.
Wasanii wengine waliotajwa kuwania kipengele hicho ni pamoja na wasanii kutoka Nigeria; Wizkid, Davido, Kcee, Patoraking na Olamide.
Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa mwaka huu nchini Marekani katika jimbo la Antalnta Georgia.