30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Desmond Tutu alazwa tena

Desmond Tutu
Desmond Tutu

Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel kutoka Afrika Kusini na Askofu wa zamani Desmond Tutu na amelazwa hospitalini kwa mara nyengine tena baada ya kupata maambukizi.

Taarifa inasema kuwa pamoja na kuwa yuko hospitali bado mtetezi huyo mkuu wa haki za binadamu na aliyepinga utawala wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini amepata, haijabainika ni maambukizi ya aina gani ambayo yanamsumbua.

Familia yake imesema maambukizi hayo hayahusiani na saratani ya tezi dume ambayo imekuwa ikimtatiza kwa takriban miaka 20.

Askofu Desmond Tutu, 84, amekuwa akilazwa hospitalini mara kwa mara katika miaka ya hivi karibuni na amekuwa akitibiwa maradhi ya saratani ya tezi dume.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles