26.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Marekani: Bunduki ruksa darasani

Guns

Wanafunzi wa vyuo katika jimbo la Texas, Marekani wameruhusiwa kuingia na bunduki darasani.

Hii ni baada ya maprofesa wawili kushindwa kwenye ombi lao la kutaka mahakama izuiwe kutekelezwa kwa sheria mpya inayowaruhusu wanafunzi kubeba bunduki bila kuzionyesha hadharani.

Jaji katika mji wa Austin alipuuzilia mbali madai ya wahadhiri hao kwamba kuwepo kwa bunduki huenda kukawa hatari kubwa iwapo mjadala mkali utazuka darasani.

Mwanasheria mkuu wa Texas, Ken Paxton, ambaye ni wa chama cha Republican, aliunga mkono uamuzi wa jaji.

Alisema raia wanaotii sheria wana haki ya kujilinda hata wakiwa kwenye vyuo vikuu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles