24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

DABA waja na mashindano ya majaribio

Na Victoria Godfrey, Dar es Salaam

Chama cha Ngumi za Ridhaa mkoa wa Dar es Salaam (DABA) umeandaa mashindano ya majaribio ambayo yamepangwa kufanyika Machi 20 mwaka huu kwenye Ukumbi wa CCM Amana, Ilala jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na www.mtanzania.co.tz Mwenyekiti wa DABA, Akalory Godfrey, amesema yatashirikisha vilabu mbalimbali jijini .

Amesema lengo ni kuwaandaa na kuwaweka tayari mabondia kushiriki mashindano ya wazi wa mkoa wa Dar es salaam yatakayoanza Aprili 7 hadi 10 jijini humo.

“Kabla ya kuelekea kwenye mashindano ya mkoa, tutaanza mashindano ya majaribio ambayo yatakuwa ni kipimo cha Makocha wa vilabu kuimarisha wachezaji wawe na ushindani,” amesema Godfrey.

Ametoa wito kwa vilabu kujitokeza kwa wingi kushiriki mashindano hayo ya majaribio.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles