30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Courtois apotezea FIFA kumtosa

MADRID, Hispania

MLINDA mlango wa Real Madrid, Thibaut Courtois, amesema haimuumizi kichwa kutokuwamo kwenye orodha ya wanaowania tuzo ya Kipa Bora wa Mwaka huu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).

Makipa waliotajwa kuiwania tuzo hiyo ni Alisson Becker, Gianluigi Donnarumma, Edouard Mendy, Manuel Neuer na Kasper Schmeichel.

Alichokisema kipa huyo tegemeo kwa Madrid na timu ya taifa ya Ubelgiji ni kwamba ameachwa kwenye tuzo hiyo kwa kuwa amekuwa akiikosoa mara kadhaa.

Baada ya majina kuwekwa hadharani, zoezi la kupiga kura lilianza Jumatatu ya wiki hii, likitarajiwa kufungwa Desemba 10, mwaka huu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles