27.5 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Corona yamweka kitanzini Rais Brazil

RIO, Brazil

MASENETA nchini Brazil wamepiga kura ya kutaka Rais Jair Bolsonaro kufunguliwa mashitaka kwa namna alivyoshindwa kuweka mikakati ya kupambana na janga la Corona.

Kwa mujibu wa kile walichokiona maseneta hao, Rasi Bolsonaro anapaswa kufikishwa kwenye mkono wa sheria kwa kosa la kupuuza maisha ya watu baada Corona kuua raia 600,000.

Hata hivyo, hofu ya wengi ni kwamba huenda lisitokee hilo la kufunguliwa mashitaka kwani Mwendesha Mashitaka Mkuu, Augusto Aras, ni miongoni mwa walioteuliwa na Rais huyo.

Mbali ya hoja hiyo ya uhalifu dhidi ya binadamu, Kamati ya Maseneta imependekeza mashitaka mengine nane dhidi ya kiongozi huyo, likiwamo la kughushi nyaraka zilizotumika kueneza taarifa zisizo sahii juu ya Corona.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles