Na Sheila Katikula,Mwanza
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mabenki kutoka Benki Kuu, Jerry Masyenene, amesema ifikapo Aprili 30, mwaka huu vikoba ambavyo havijasajiliwa havitatambulika katika sekta ya fedha.
Masyenene amebainisha hayo katika ufunguzi wa mafunzo ya miongozo na mfumo wa usajili wa vikundi vya kijamii vya huduma ndogo za fedha uliofanyika mkoani Mwanza.
Akizungumza na Maafisa Tehama na Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka Mikoa ya Mwanza, Kigoma na Shinyanga amesema agizo hilo linazingatia sheria mpya ya huduma za fedha ya mwaka 2018 benki kuu ndiyo maana imetoa mafunzo hayo kwa maafisa hao.
Amesema faida za kusajili vikoba ni pamoja na kupunguza wimbi la umasikini katika jamii,kutengeneza mamilionea na kupata mikopo kwa haraka kutokana na kutambulika katika sekta za kifedha.
Amesema kila kikundi kinapaswa kuwa na wanachama wasiopungua 10 na wasiozidi 50 tofauti na hapo hakitasajiliwa, hakuna gharama ya usajili na kila kikundi kitatakiwa kuwa na katiba ambayo imepitishwa kwenye mkutano Mkuu mmoja na kutakuwa na mkaguzi wa kikundi na ukaguzi kutoka Tamisemi.
“Na baada ya usajili watapewa cheti kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kupitia vikundi hivyo tutapata mabilione kwani huko nyuma walikuwa wakitapeliwa fedha zao kwa sababu ya kukosa mfumo wa kielektroniki  kupitia  sheria  hiyo ya usajili wa vikundi utawaweka salama ili kuendelea kunufaika  kwenye vikundi vyao.
Amesema huko nyuma kulikuwa na makampuni mengi yanayotoa mikopo lakini hakukuwa na usimamizi wowote kwani hivi sasa kampuni zote zinazotoa mikopo zipo chini ya usimamizi wa banki kuu kwani imetengeneze nyaraka zote muhimu zitakazosimia vikundi hivyo.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanel Kipole, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela amewata Maafisa Maendeleo ya Jamii Maafisa Tehama kuwashirikisha elimu waliyoipata watendaji wa kata, mtaa navijiji kwa  sababu vikundi hivyo huanzia huko no vema kuhakikisha zoezi hilo linasimamiwa ili kupunguza kiwango cha umasikini kwenye  Maene yao.