Jestina John(TUDARco) na Mashirika
Rais wa Marekani, Joe Biden amezungumza leo Jumanne Agosti 17, 2021 na kutetea msimamo wake wa kuondoa wanajeshi wa Marekani katika nchi ya Afghanistan. Hii ni baada ya wanajeshi wa Afghanistan kutelekeza nchi kwa wanamgambo wa Taliban.
Rais Biden ametoa tamko na kujibu uvumi unaosemwa dhidi yake kuwa amekosea kuyaondoa majeshi ya Marekani nchini humo kwa kusema wanajeshi wa Marekani hawatakiwi na hawatatakiwa kipigania vita na kufa kwenye vita ambayo wanajeshi wa Afghanistan wenyewe hawajitoi kupigania nchi yao
Biden amesema wanajeshi wa Afghanistan wamepewa mafunzo na wamarekani ingawa wanashindwa kupambana na wanamgambo hao