24.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

BET kumpa Mary J Blige tuzo ya heshima

LOS ANGELES, MAREKANI

MWANAMUZIKI mkongwe wa miondoko ya Pop na RnB, Mary J. Blige, anatarajia kutunukiwa tuzo ya heshima (Lifetime Achievement Award) kwenye tuzo za BET zitakazofanyika June 23-25, mwaka huu katika ukumbi wa Microsoft Theater, Los Angeles, Marekani  .

Mary J, ambaye aliwahi kuwa mshindi wa tuzo za Grammy mara tisa pamoja na kuuza album zake mara nane (multi-platinum) atatunukiwa heshima hiyo kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa kwenye tasnia ya muziki tangu mwaka 1992.


Imeelezwa kuwa, Mary J Blige ataungana na waimbaji kama Anita Baker wa mwaka jana, pia Charlie Wilson, Diana Ross, Whitney Houston, New Edition, James Brown na Prince wakiwa miongoni mwa mastaa waliopokea tuzo hiyo ya heshima.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles