23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Beka: Mwaka huu ni wa bendi na albamu

beka-559x520NA GLORY MLAY

MKALI wa muziki wa kizazi kipya, Bakari Hassan maarufu kwa jina la (Beka), ameweka wazi kuwa kwa mwaka huu amepanga kuitambulisha bendi yake mpya ya Spidoch na ujio wa albamu yake ya kwanza.

“Mpango wangu mkubwa kwa mwaka huu ni kuwekeza katika bendi yangu kuanzia uzinduzi wake, aina ya utumbuizaji na namna tutakavyokuwa tunafanya kazi pamoja na mashabiki wetu.

“Lakini pia nitatambulisha albamu yangu ya kwanza ambayo naamini itakuwa ya kisasa na itauzika tofauti na wengi wanavyodai albamu haziuzi lakini ya kwangu itauza kutokana na namna nilivyoweza kutafuta soko lake,” alisema Beka.

Barnaba ndiye msanii ambaye amerudia wimbo unaoongoza kwa kusikilizwa na mashabiki wengi duniani wa ‘Hellow’ wa Adele ambao ameuimba kwa ustadi mkubwa licha ya kuwepo kwa makosa machache ya kiutamshi wa baadhi ya maneno ya Kiingereza ambayo anadai imetokana na kutokujua lugha hiyo kwa ufasaha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles