28.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Baby J: Siringi mnanichukia bure

Jamila Abdallah  ‘Baby J’
Jamila Abdallah ‘Baby J’

NA THERESIA GASPER

MMOJA wa wasanii wa Zanzibar watakaotumbuiza katika Tamasha la Filamu la Kimataifa (ZIFF), Jamila Abdallah  ‘Baby J’, amewataka wanaomchukia na kudhani kwamba anadharau wabadilishe mitazamo yao kwa kuwa yeye ni mtu wa kawaida mwenye tabia za kuzungumza na kujichanganya na watu wa rika zote.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Baby J alisema anapenda kushirikiana na amejiwekea tabia za kuzungumza na kila mtu tofauti na baadhi ya watu wanavyomtafsiri.

“Watu wengi wanaona wasanii huwa tunaringa au tunadharau kutokana na kazi zetu kitu ambacho kwangu si sahihi kwa kuwa napenda ushirikiano na kila mtu,” alisema.

Msanii huyo alisema mbali na kazi yake ya muziki vile vile amejikita katika biashara ya vipodozi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles