24.2 C
Dar es Salaam
Sunday, April 28, 2024

Contact us: [email protected]

Azam tv yazindua tamthilia mbili za moto

Na Beatrice Kaiza, Mtanzania Digital

KAMPUNI ya Azam Media imetambulisha tamthilia mbili za Kitanzania zinazofahamika kama ‘Mtaa wa Kazamoyo na Lolita’ ambazo zimebeba simulizi na kuleta mapinduzi ya tasnia ya tamthilia nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari, juzi jijini Dar es Salaam, Msimamizi Mkuu wa Chaneli ya Sinema Zetu, Sophia Mgaza amesema kuwa uzalishaji wa tamthia hizo mbili zimezingatia mahitaji ya soko kwani wametumia vifaa vya uzalishaji wa kisasa na ubora wa hali ya juu,” amesema Mgaza.

Aliongezea kwa kutoa rai jwa waandaaji wapya wanaongia na kazi zao za sanaa zinazoruka kwenye chaneli hiyo waweze kuhakikisha wanasimamia ubora wa kazi ili wasije kutoa sababu kwa watu wa pembeni kuwanyooshea vidole na kusema kuwa ilikuwa ni nguvu ya soda tu,” amesema Mgaza.

Pia amesema tamthilia hizo zinachukua nafasi ya Fungu langu itakayofikia tamati Julai 29, 2023 na Jeraha itakayofikia tamati tarehe 10 Agosti, 2023.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles