23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Aomba msaada kudhibiti tembo

tembo

Na RAPHAEL OKELLO,

MKURUGENZI  wa Halmashauri  ya Mji wa Bunda, Janet Mayanja ameiomba Wizara ya Maliasili na utalii  kuangalia uwezekano  wa kuwadhibiti tembo kutoka ndani ya Hifadhi Taifa ya Serengeti.

Amesema wanyama hao wamekuwa wakiharibu mali za wananchi  ndani ya mji wa Bunda.

Mayanja alisema  hivi sasa wimbi la tembo kutoka katika hifadhi hiyo na kuvamia makazi ya watu limekuwa kubwa na kuongezeka  kwa kasi.

Alisema  Wizara ya Maliasili inapaswa kufikiri kwa kina au kufanya utafiti wa nini kifanyike ili kutatua jambo hilo.

“Ni kweli tembo hawa  wanaharibu  mali za wananchi  lakini mbaya zaidi  wananchi wale ambao bado wanategemea  kilimo pembezoni  mwa mji, mazao yao yanaharibika   na kuwasababishia baa la njaa.

“Tunaiomba Wizara  ya Maliasili kuangalia ni namna gani tembo hawa wanaweza  kudhibitiwa, sisi kama halmashauri  tunafanya kila tunaloweza katika kukabiliana na janga hili lakini nguvu yetu ni ndogo.

Katika  siku za hivi  karibuni  makundi  ya tembo  yaliwavamia  makazi ya wananchi   wa vijiji vya Nyatare, Kunzugu, Tamao na  Nyatware, katika halmashauri  ya mji huo   kuvunja  ghala  na  kula mazao ya akiba yaliyohifadhiwa na wananchi hao.

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Charles Mlingwa  alisema   serikali inalifanyia kazi  tatizo hilo la tembo na wanyama pori wengine wanaofanya uharibifu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles