25 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Rais Santos ‘mahakamani’ kwa tuhuma za upendeleo Angola

Rais wa Angola, Jose Eduardo dos Santos
Rais wa Angola, Jose Eduardo dos Santos

LUANDA, ANGOLA

MAHAKAMA ya Juu ya Angola imemuamuru Rais Jose Eduardo dos Santos kujibu tuhuma za kumteua binti yake Isabel kuongoza Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Sonangol.

Dos Santos alimteua binti yake huyo bilionea kuwa mtendaji mkuu wa kampuni hiyo Juni mwaka huu.

Uamuzi huo wa mahakama umetokana na kuanza kuyafanyia kazi maombi ya shauri lililowasilishwa mahakamani hapo na wanasheria 14 wa Angola.

Wanasheria hao wanaomtuhumu kiongozi huyo mkongwe nchini hapa kuendekeza undugu na kuvunja sheria ya uaminifu ya nchi hiyo.

Hata hivyo, si rais mwenyewe, msemaji kutoka kitengo cha mawasiliano cha Ikulu wala Isabel mwenyewe, aliyepatikana mapema wala kupokea simu kuzungumzia mwito huo wa mahakama.

Isabel, ambaye ni bilionea namba moja mwanamke barani Afrika kwa mujibu wa Jarida la Forbes la Marekani, aliteuliwa kuchukua mamlaka hayo mara baada ya hatua ya kushtukiza ya baba yake kuivunja Bodi ya Sonangol.

Miongoni mwa hatua, ambazo Isabel aliahidi kuzichukua dhidi ya kampuni hiyo ni pamoja na kuigawanya katika vitengo vitatu; uzalishaji, usafirishaji na kitengo kitakachohusika na mikataba.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles