31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

AMBER ROSE: NITARUDI KWENYE UBORA WANGU

LOS ANGELES, MAREKANI


MREMBO Amber Rose ametumia mitandao yake ya kijamii kuwaambia mashabiki zake kwamba, atarudi kwenye ubora wake mara baada ya kufanikisha upasuaji wa matiti.

Mwanamitindo huyo Jumanne ya wiki iliyopita, alifanyiwa upasuaji wa matiti yake kwa ajili ya kuwa kwenye mwonekano wa kisasa zaidi.

Amber aliwahi kusema kwamba, anachukia mwonekano wake kwa kuwa matiti yamekuwa makubwa, hivyo alilazimika kufanyiwa upasuaji ili kuyapunguza kwa ajili ya kupendeza zaidi.

“Nilikuwa sina raha sana kuwa na matiti makubwa, lakini ninaamini baada ya upasuaji nitarudi katika ubora wangu kama ilivyo zamani, mashabiki wangu wakae tayari kuniona nikiwa na mwonekano tofauti,” alisema Amber.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles