22.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

African Lyon yarejea Ligi Kuu Bara

african lynoNA MSHAM NGOJWIKE, DAR ES SALAAM

TIMU ya soka ya African Sports imerejea katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara licha ya kutoka sare ya bao 1-1 na Ashanti United, katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) uliochezwa jana katika Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Matokeo hayo yameiwezesha timu hiyo kuongoza katika kundi A kutokana na pointi 29 walizojikusanyia huku Ashanti wakishika nafasi ya pili kwa kufikisha pointi 24.

Katika mchezo huo, African Lyon walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya tatu lililofungwa na Omary Abdallah kwa shuti kali.

Ashanti United walisawazisha dakika ya 50 kupitia kwa Mwini Ally ambaye alifanikiwa kuwatoka mabeki wa African Lyon na kuachia shuti lililojaa wavuni.

African Lyon imeungana na Ruvu Shooting kurejea Ligi Kuu baada ya kushuka daraja, huku Geita Gold ikipata nafasi ya kupanda daraja kwa mara ya kwanza baada ya kuongoza katika kundi C.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles