24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Adakwa akipiga kura mara mbili

PRETORIA, Afrika Kusini

MWANAUME mkazi wa mjini Mamelodi, Afrika Kusini, ameingia kwenye mkono wa jeshi la polisi baada ya kunaswa akijaribu kupiga kura mara mbili katika uchaguzi mdogo unaoendelea nchini humo.

Tukio hilo lilitokea katika kituo cha Shule ya Msingi ya Sindawonye na aliyemnasa ni wakala wa moja ya vyama vya siasa, ambaye hata hivyo hakutaka jina lake lianikwe kwenye vyombo vya habari.

Akisimulia ilivyokuwa, wakala huyo amesema jamaa alifika kituoni hapo asubuhi, ambapo alipiga kura na kuondoka zake.

Kwa mujibu wa wakala, mwanaume huyo alirejea jioni na ndipo ‘janjajanja’ yake ilipomponza. “Nilishaangaa nilivyotazama kitambulisho chake na kukuta alishapiga kura,” amesema wakala.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles