27 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Mke amfanyia ‘kitu mbaya’ staa wa soka

PRETORIA, Afrika Kusini

MPACHIKAJI mabao wa zamani wa Orlando Pirates, Tendai Ndoro, amejikuta akipoteza mali zote alizochuma baada ya kukorofishana na mkewe aitwaye Thando Maseko.

Katika kilele cha penzi lao, Ndoro aliyewahi pia kung’ara akiwa na timu ya taifa ya Zimbabwe, aliandikisha jina la bibiye huyo kwenye mali zote, yakiwamo magari na nyumba.

Sasa, kilichotokea ni kwamba wawili hao wametibuana na alichokifanya bi. Thando ni kumfukuza mshikaji kwenye mjengo waliokuwa wakiishi, ikizingatiwa kuwa ndiye jina lake linalotumika kwenye umiliki.

Taarifa za Ndoro ‘kufulia’ zilianza kusambaa nchini Afrika Kusini hivi karibuni baada ya mwanasoka huyo kuonekana akiwa amepungua uzito, ambapo ilielezwa kuwa huenda anasumbuliwa na tatizo la akili.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles