25.6 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 30, 2024

Contact us: [email protected]

Nape azungumzia tukio la kutishiwa bastola kwa mara ya kwanza

Na Maregesi Paul

Mbunge wa Mtama,Nape Nnauye amezungumzia kwa mara ya kwanza tukio lake la kutishiwa bastola miaka miwili iliyopita.

Katika maelezo yake, Nape amsema wakati anatishiwa kwa bastola miaka miwili iliyopita  walikuwapo watu mbalimbali akiwamo Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD)pamoja na Kamanda wa polisi wa Mkoa (RPC).

Pamoja na hayo alishangaa tukio lake hilo kutotolewa ufafanuzi wowote na Serikali wakati inalijua vizuri.

Nape aliyasema haya bungeni wakati Bunge lilipokaa kama Kamati ya Matumizi kujadili bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Aidha Nape aliitaka Serikali ijitenge na matukio ya kihalifu kama ya tukio lake kwa kuwa anaamini aliyemtishia hakutumwa na Serikali ingawa anamfahamu vizuri.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles