27.2 C
Dar es Salaam
Friday, September 20, 2024

Contact us: [email protected]

Wakazi Kigoma washauriwa kuwekeza Hati Fungani

Na Mwandishi wetu, Kigoma

Wananchi Mkoani Kigoma wametakiwa kujenga utamaduni wa kuwekeza fedha zao kwa kununua Hati Fungani mbalimbali zinazouzwa na Serikali ili iwe moja ya vyanzo vya kujiongezea vipato badala ya kuweka fedha zao katika mfumo usio rasmi.

Akizungumza na timu ya watalaamu kutoka Wizara ya Fedha, Katibu Tawala Mkoa Kigoma, Hassan Kaigwa amesema uzoefu unaonyesha watu wengi wanaonunua Hati Fungani za Serikali hunufaika kwa kupata faida muda mfupi huku mtaji wao ukiendelea kuwepo na kutoa wito kwa wananchi wanaomiliki fedha kuchangamkia fursa hiyo.

Timu hiyo imeanza ziara ya kutoa mafunzo kwa wananchi kwa makundirika mbalimbali Mkoani Kigoma ili kuwajengea uwezo na kutambua fursa za kuwekeza, kujiongezea kipato, kufanya uwekezaji na kujiwekea akiba.

“ Katika Hati Fungani za serikali kwa mwaka unaweza kupata faida kati ya asilimia 12 hai 15 ambapo kwa mtu aliyenunua bondi za thamani ya shilingi million 200 anauwezo wa kupata zaidi ya shilingi milioni 24 kwa mwaka huku mtaji wake ukiwa pale pale, mzunguko huu wa fedha sio jambo la kulipuuzia hivyo ni muhimu kila mwananchi achangamkie fursa hii adhimu,” amesema Kaigwa.

Amesema kuwa sio lazima watu wote wawe wafanyabiashara bali wengine wanaweza kuwa wadau au wabia wa benki ama uwekezaji ili wanaojua kufanya biashara wafanye shughuli hiyo kwa kutumia fedha za wale wasiojua kufanya biashara wakaamua kuwekeza.

Ofisa Usimamizi wa Fedha Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha Wizara ya Fedha, Stanley Kibakaya, amesema kutokana na umuhimu wa elimu ya fedha katika kuwakomboa wananchi katika umaskini, Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi Dk. Samia Suluhu Hassan, imeamua kuweka mkazo wa kutoa elimu ya fedha kwa wananchi ili waweze kunufaika.

Kibakaya amesema kuwa mpaka sasa Rais Samia Suluhu Hassan, ametoa maelekezo kwa Wizara ya Fedha kutumia watalaam wake wazunguke nchi nzima kutoa elimu kwa wajasiriamali, wakulima na watumishi wa umma kuwajengea uwezo wa mambo muhimu ya kuzingatiwa kwenye elimu ya fedha ikiwemo umuhimu wa uwekezaji na namna ya kulinda mitaji

“Ndio wakati muafaka sasa ambapo Serikali yetu imeona kupitia huu mtaala mpya wa elimu ya fedha ifundishwe kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu na Wizara imepokea maelekezo kupitia Mhe.Rais kuhakikisha tunapita katika mikoa yote kuwapatia elimu wananchi wote ambao hawakufanikiwa kuipata katika mfumo rasmi,”amesema

Kibayakaya amebainisha kuwa katika kutekeleza agizo la Rais tayari awamu ya kwanza imekwishafanyika na sasa ni awamu ya pili imeanzia mkoani Kigoma ambapo jumla ya Halmashauri nne zitafikiwa na mpango huo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles