23.6 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Xhaka ataka kurudi Bundesliga

LONDON, England

KIUNGO wa Arsenal, Granit Xhaka, anavutiwa na mpango wa kurejea katika klabu yake ya zamani ya Borussia Monchengladbach.

Lakini, Xhaka raia wa Uswis mwenye umri wa miaka 26, anataka hilo litokee pale atakapomaliza mkataba wake na Arsenal mwaka 2024. 

Nyota huyo amekuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Washika Bunduki tangu aliposajiliwa mwaka 2016, ambapo ameshashuka dimbani mara 225.

Hata hivyo, kiwango chake kimekuwa kikishuka mara kadhaa na itakumbukwa alikaribia kuuzwa mwaka jana, kabla ya kupewa mkataba wa miaka mitatu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles