24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

WIMBO WA DIAMOND, RICH MAVOKO WACHUNGUZWA

screenshot-from-2016-07-01-134855
Diamond Platnumz

Video ya wimbo mpya wa ‘Kokoro’ ulioimbwa na wasanii wa Bongo Fleva kutoka kundi la Wasafi, Richard Martin (Rich Mavoko) na Nassib Abdul (Diamond Platnumz), unachunguzwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Bodi ya Filamu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kama video hiyo ina udhalilishaji wa mwanamke au la.

Mkuu wa matukio wa Baraza hilo, Kurwijira Maregesi, amesema kwamba wanafanyia uhakiki wa video hiyo kutokana na baadhi ya vipande katika video hiyo kuonyesha udhalilishaji wa mwanamke, tabia ambayo inapingwa vikali na jamii.

“Katika kusimamia maadili ya sanaa na udhalilishaji wa wanawake, tuko thabiti kuhakikisha hakuna msanii anayepotosha taifa wala kumdhalilisha mtu,” alisema Maregesi

Maregesi aliongeza kwamba kumekuwa na tabia kwa wasanii wa Bongo fleva kutoa nyimbo zenye kupotosha Taifa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles