26.2 C
Dar es Salaam
Friday, May 3, 2024

Contact us: [email protected]

Watanzania watakiwa kuwa wazalendo

Na Hadia Khamis, Mtanzania Digital

Watanzania wametakiwa kuwa wazalendo katika kushiriki Sensa ya Watu na Makzi itakayofanyika Agosti 23, mwaka huu ili kuweza kufanikisha mipango ya serikali.

Hayo yamebainishwa Dar es Salaam leo Agosti 16, 2022 na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Hassan Abbas wakati wa uzinduzi wa tamasha la Sensabika.

“Kama wizara tulizindua awamu ya kwanza ya Sensabika ambayo ilikuwa Kidigital zaidi hii yote ni kumuunga mkono Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema Dk. Abbas.

AMesema Agosti 21, mwaka huu wanatarajia kufanya tamasha la aina yake ambalo halijawahi kufanyika nchini.

meongeza kuwa tamasha hilo kubwa ni kuhamasisha wananchi kuweza kushiriki katika Sensabika kwa kushiriki katika michezo mbalimbali.

Amesema tamasha hilo linatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam kuanzia saa 12 Asubuhi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles