21.5 C
Dar es Salaam
Saturday, July 27, 2024

Contact us: [email protected]

Watainiwa 2,677 kufanya mtihani wa kidato cha Nne Bukoba

Renatha Kipaka, Bukoba

WATAHINIWA 2,677 katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wanatarajia kuanza mtihani wao wa kuhitimu kidato cha nne kesho Novemba 15, mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumapili Novemba 14, 2021 na Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Bukoba, Hamid Njovu wakati akizungumza na Waanahabari ofisini kwake.

Amesema, kati watahiniwa hao wavulana ni 1,292 na wasichana ni 1,385 huku vituo vya kufanyia mtihani vikiwa 37.

“Hivi vituo vipo kwa makundi matatu kuna shule za serikali 17, shule za binafsi 13 na wale wa kujitegemea 7, wote wameandaliwa kwa mujibu wa Sheria,” amesema Njovu.

Aidha, amesema kuwa katika idadi hiyo watu wenye ulemavu watakapo fanya mtihani uoni hafifu 2, Viziwi 9, ulemavu wa viungo 4 ambao jumla yao ni 15.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles