21.5 C
Dar es Salaam
Saturday, July 27, 2024

Contact us: [email protected]

Watafiti mazao ya uvuvi watakiwa kuja na suluhisho soko la kimataifa 

Na Clara Matimo, Mwanza

Watafiti  wa mazao ya uvuvi wametakiwa kutoa  matokeo yenye tija  yatakayowawezesha wananchi kunufaika na masoko ya nje ya nchi.

Wito huo umetolewa jijini hapa Aprili 19,2023 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Balandya Elikana kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Adam Malima alipomwakilisha kwenye ufunguzi wa    warsha ya wadau  wa mazao ya uvuvi iliyolenga  kupokea na kupitisha taarifa ya utafiti kuhusu upotevu wa mazao ya uvuvi nchini.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanz,a Balandya Elikana akizungimza kwenye mkutano huo.

Amesema ingawa kwa mujibu wa utafiti uliofanyika mwaka 2020 umeonesha  kiwango cha uvuvi wa dagaa kiko juu kwa asilimia 45 ukilinganishwa na sangara ambao una asilimia 33 lakini  haujawa na tija ya kuinua kipato cha wananchi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa soko la uhakika.

 “Lazima tujiulize kwa nini uvuvi wa dagaa hauna tija kubwa hivyo tunahitaji watafiti wa mazao ya uvuvi mfanye utafiti mje na suluhisho ili dagaa zinazovuliwa ziandaliwe kisasa katika hatua zote kuanzia zonapovuliwa hadi zinapoingizwa sokoni twende na wakati ili dagaa zetu ziwe bora zikidhi vigezo vya soko la kimataifa ili ziinue uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

 “Hata hivyo naipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI)  kwa kufanya utafiti huo wa mwaka 2020 hasa  katika mazao ya dagaa  hivyo ni matumaini yangu kwamba utapunguza changamoto  zilizopo au kuzimaliza kabisa,” amesema Elikana

 Kaimu Mkurugenzi wa TAFIRI, Hilary Mroso amebainisha kwamba kwa ya kuimarisha mnyororo wa thamani kwa kusimamia njia zote bora na za  kisasa kwa mazao ya uvuvi ili kulinda usalama wa mazao hayo baharini na kwenye maziwa.

 “Tutaendelea kufanya utafiti kama huo ili kuhakikisha taifa linakuwa salama kwa chakula na wananchi kwa ujumla, tunashukuru nchi yetu kupata nafasi ya kuteuliwa na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO)kufanya utafiti.

“FAO  limeziteua nchi tatu ikiwemo Tanzania, Sri Lanka na Colombia kutoka mabara matatu ya Afrika, Asia na Latin Amerika kuhusika na utafiti wa upotevu wa mazao ya uvuvi kwa lengo la kupata ufumbuzi, nini kifanyike na kuwepo mikakati endelevu ya usalama wa mazao hayo kwa udhamini wa Serikali ya Norway,” amesema Mroso.

Kwa mujibu wa Mroso utafiti huo umefanyika Bahari ya Hindi, Ziwa Victoria na Nyasa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles