25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Wasomi wachambua kauli ya Prof. Ndulu

Profesa Benno Ndulu.
Profesa Benno Ndulu.

JONAS MUSHI Na LEONARD MANG’OHA, DAR ES SALAAM

SIKU moja baada ya Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Benno Ndulu kueleza kuwa hali ya uchumi iko imara, wasomi na wachumi wameibuka wakisema amerudisha imani iliyopotea na kwamba wananchi wawe wavumilivu.

Kwa wiki moja sasa kumekuwa na mjadala kuhusu hali ya uchumi, huku wachambuzi na wanasiasa wakielezea hali ya maisha ilivyo ngumu kutokana na fedha kupotea mikononi mwa watu.

Miongoni mwa wanasiasa waliochambua hali ya uchumi ni Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe ambaye alisema kuwa kumekuwapo na mdororo wa uchumi ikilinganishwa na mwaka jana.

Pia Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, akiwa bungeni wiki iliyopita, alielezea namna deni la taifa lilivyopanda huku hali ya maisha ikiendelea kuwa ngumu.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles