23.3 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Wanawake waongoza maambukizi VVU Buchosa

Anna Ruhasha, Mwanza

TAKWIMU za kuanzia Septemba, 2019 hadi Oktoba mwaka 2020 za maambukizi mapya ya Virusi vya UKIMWI (VVU) katika Halmashauri ya Buchosa iliyopo Wilayani Sengerema mkoani Mwanza ni asilimia 7.7 kiwango ambapo wanawake wameogoza.

Taarifa hizo zimetolewa na Mratibu wa UKIMWI katika Halmashauri hiyo, Frolian Mkangara, ambaye amesema  wanaoishi na  VVU katika Halmashauri ya Buchosa wanakadiriwa  kuwa 17,795, wanaume  kuanzia umri wa miaka 15 ni 6,390 na wanawake  umri kuanzia miaka 15 ni 9,807 .

Aidha ameongeza kuwa watoto chini ya miaka 15  waliogundulika na VVU wakiume walikuwa  1,627 na wakike  1,385  na vituo 37 vimeweza kutoa huduma za upimaji na dawa za kufubaza  makali ya VVU bure.

“Pamoja na takwimu hizo mgeni rasmi bado wanawake katika Halmashauri ya Buchosa wanaongoza  hasa kuanzia umri wa  miaka 24 -49 kulinganisha  na wanaume wa umri huo,”amesema.

Kwa upande wake Mkurungenzi wa Halmashauri ya Buchosa, Paulo Malala  ametumia Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani kuitaka jamii kupima afya zao kila mara na kuchukua tahadhari kwa kutumia kinga.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti Ukimwi ambaye ni Diwani wa Kata ya Katwe, Maximilian Laurenti, amesema kuwa licha ya kundi la wanawake kuongoza  takwimu za kuanzia maambukizi yameshuka  kutoka asilimia 7.7 na kufikia asilimia 4.5 .

“Takwimu za kuanzia mwezi Oktoba  2020 hadi September 2021  jumla ya  wananchi wapatao 42,395, wanawake 24, 299  na wanaume  18,096 kati yao waliogundulika na VVU wanawake ni 1,101 na wanaume 795 na kushusha kiwango cha maambukizi  kufika asilimia 4.5” amesema Laurent

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles