23 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Wafanyabishara Mwanza watafakari kugoma

Jiji la Mwanza
Jiji la Mwanza

NA BENJAMIN MASESE

JUMUIYA ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) mkoani Mwanza imewatangazia wafanyabiashara kutofunga maduka badala yake kungoja maelekezo ya vikao.

Akizungumza na gazeti jana, Mwenyekiti wa JWT mkoa wa Mwanza, Christopher Wambura, alisema wafanyabiashara hawatafunga maduka yao kwa kuwa  vikao vinaendelea sasa.

Tamko la JWT limetolewa ikiwa ni siku moja baada ya TRA na polisi kutoa tangazo la kusisitiza matumizi ya mashine EFD’s.

TRA pia imewaonya wale wanaohamasisha   kuwarubuni wafanyabiashara kutotumia  mashine hizo.

Taarifa ya TRA na polisi   imeonya  watakaokiuka  au kuhamasisha mgomo juu ya matumizi ya mashine ya EFD watachukuliwa hatua za sheria kwa kuwa ni kosa  la jinai.

Wambura alisema wameanza vikao vya ndani kujadili jinsi ya  kukabiliana na matakwa ya TRA na polisi kutumia mashine za EFD wakati bado hakuna makubaliano yaliyofikiwa kama alivyoelekeza Rais Jakaya Kikwete Aprili 22, mwaka huu alipokuwa  Karatu mkoani Arusha akifungua ofisi za TRA.

“Sisi hatuna nguvu ya kupambana na vyombo vya Serikali ambavyo vinavyotaka  matumizi ya mashine hizo.

“Silaha tuliyobaki nayo ni umoja wetu  kama ulivyoona jana (juzi) wafanyabiashara wa Dar es Salaam walifunga maduka yao.

“Hapa Mwanza tumewaeleza wasifunge maduka yao ila sisi viongozi tunaanza vikao vya ndani kupanga namna ya kupambana na matakwa ya TRA na polisi, siku tukitangaza mgomo utakuwa ni nchi nzima,”alisema.

Mgomo wa wafanyabiashara nchini dhidi ya mashine za EFD ulianza  Desemba mwaka jana na umekuwa ukisimamishwa kwa muda huku Serikali ikifanya mazungumzo na wafanyabiashara hao ingawa hadi sasa haujapatikana mwafaka.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles