31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

TRILIONI 1.2 HUTUMIKA KUDHIBITI UKIMWI KWA MWAKA

Na Hamisa Maganga, Bagamoyo

Tanzania hutumia Sh trilioni 1.2 kwa ajili ya shughuli za kudhibiti Ukimwi kwa mwaka.

Aidha, asilimia 93 ya fedha za kudhibiti Virusi vya Ukimwi (VVU) hutolewa na wahisani ambapo kati ya hizo asilimia 86 hutoka Marekani.

Mkurugenzi wa Fedha na Utawala kutoka Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bara (TACAIDS), Yasin Abbas, amesema hayo leo Alhamisi Machi 8, wilayani Bagamoyo wakati akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari kuhusu uandaaji wa programu bora za VVU na Ukimwi.

Amesema asilimia kubwa ya fedha hizo hutumika katika kununua dawa za kufubaza makali ya VVU (ARVs).

“Asilimia 93 ya fedha hufadhiliwa na wadau wa maendeleo kutoka nje ya nchi, kati ya hizo asilimia 86 zinatoka Marekani kupitia programu yake ya PEPFAR na Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund ATM).

“Tanzania hutoa asilimia saba tu ya fedha zote. Hivyo, kupitia Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (ATF), tunatarajia kuongeza rasilimali za ndani kutoka asilimia saba mwaka 2015 hadi asilimia 30 mwaka huu,” amesema Abbas.

Hata hivyo, amesema iwapo watafanikiwa kufikia lengo, Tanzania itaondokana na utegemezi kwa asilimia kubwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles